Ushauri huo umetolewa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma utafiti na ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala wakati akifungua mafunzo ya siku nne kwa wanataaluma wachanga wa Chuo hicho juu ya namna ya kuandika maandiko kwaajili ya kuomba fedha za kufanya tafiti.
“Tusifanye tafiti kwaajili ya kupanda madaraja au vyeo kwenye kazi zetu bali tufanye tafiti ambazo zinaweza kwenda kujibu changamoto mbalimbali zinazoikabili nchi na Jamii yetu, kwa namna hiyo ndio mtakuwa mmefikia lengo hasa la kufanya utafiti” Alieleza Prof. Mwatawala.

